Wednesday, August 13, 2014

KIBONDE, GARDNER WAPANDISHWA KIZIMBANI


Watangazaji Ephraim Kibonde (wa kwanza kushoto) na mwenzake Gardner Habash (wa pili kulia) wakielekea kizimbani.
Watangazaji hao wakiongozwa na maofisa wa polisi kuelekea mahakamani.
...Wakiingia mahakamani.
MTANGAZAJI wa Clouds FM, Ephraim Kibonde na mwenzake, Gardner Habash wa Times FM leo wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa kusababisha ajali na kudharau amri ya polisi na kutoa lugha ya matusi.
Watangazaji hao wamesomewa mashitaka hayo na Wakili wa Serikali, Salim Mohammed mbele ya Hakimu Aniseta Wambura.
Kibonde na Gadna wanadaiwa kutenda makosa hayo Jumamosi ya Agosti 9, mwaka huu saa 12 asubuhi, katika eneo la Makumbusho, ambapo Kibonde akiwa anaendesha gari walilokuwa wamepanda aliligonga gari la raia mmoja wa kigeni (Mzungu) na kukimbia.
Kesi yao imeahirishwa mpaka Septemba 10 mwaka huu itakaposikilizwa tena.(Picha na Shakoor Jongo / GPL)

MAGAZETI JUMATANO 13/08/2014

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

BIA YA CASTLE LITE YAZINDUA PROMOSHENI YA “LITE UP THE WEEKEND”

 Meneja msaidizi wa Castle Lite, Victoria Kimaro akizungumza katika uzinduzi wa kampeni ya shindano la Lite Up The Weekend ambapo washindi watajipatia VIP tiketi ya kushiriki katika Yacht Party. Katikati ni Meneja wa Castle Lite Geofray Makau na pembeni ni meneja masoko wa Castle Lite Vimal Vaghmaria.
 Wanahabari wakielekea eneo la maegesho ya Yacht itakayotumika katika kilele cha cha kampeni ya Lite Up The Weekend.
Muonekano wa Yacht itakayoandaliwa maalum kwa ajili ya washindi wa shindano la Lite Up the weekend. 
 Mmoja ya wadau wadau wa Castle Lite katika pozi ndani ya Yacht.
 Meneja masoko wa Castle Lite Vimal Vaghmaria na Stanley Kafu wa Aggrey & Clifford wakifurahia ndani ya Yacht.
 Wanahabari katika pozi la pamoja na wadau wa Castle Lite.
Dar es Salaam, Aug 11, 2014:
Bia maarufu ya Castle Lite, inayozalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) leo imezindua rasmi promosheni ya aina yake itakayojulikana kama “Lite Up The Weekend”. Promotion hii ya aina yake hapa nchini itadumu kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi Agosti hadi Octoba 2014.
Akizungumza katika uzinduzi huo, meneja wa Bia ya Castle Lite Geoffrey Makau alisema; Bia ya Castle Lite kwa mara nyingine tena inawaletea wapenzi wa bia hii habari nzuri na za kuvutia. Leo tunazindua promosheni kubwa itakayojulikana kama “Lite Up The Weekend”.
Hii ni promosheni kubwa itakayoendeshwa nchi nzima. Washindi watashiriki kwenye hii promosheni kupitia chupa za bia ambazo watatakiwa kutuma nambari ya siri iliyochini ya kizibo cha bia ya Castle Lite.
 Tumewaandalia wateja wetu zawadi mbalimbali zitakazokuwa zikitolewa kila wiki, ikiwa ni pamoja na zawadi za pesa taslimu, zawadi za vifaa vya kusikilizia muziki (headfone) n.k, lakini zawadi kubwa zaidi ni ile ya washindi kupata fursa ya kusherehekea kwenye VIP Party ndani ya Boti ya kifahari. Sherehe hii itajulikana kama “Castle Lite VIP Yacht Party”
Mteja atatakiwa kununua bia ya Castle Lite ya chupa yenye ujazo wa mililita 375 au 330 na kuangalia chini ya kizibo cha Bia, ambapo atakuta namba za siri, kisha atatuma namba hizo kwenda 15499 au kutembelea website yetu ambayo ni, www.castlelite.co.tz, ili apate nafasi ya kushinda zawadi za kila wiki au zawadi kubwa ya “Castle Lite VIP Yacht Party”.
Washindi wa zawadi kubwa kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania, watapata fursa yakuparty na wenza wao  kwenye  boti la kifahari aina ya yacht, ambayo itaondoka Dar kuelekea kisiwa kizuri kilicho andaliwa kwa ajili yao, huku wakiburudishwa kwa chakula, vinywaji na muziki 
Promosheni hii pia itapewa msukumo mkubwa kupitia Radio, ambapo wapenzi wa Castle Lite watapigiwa simu na watatakiwa wapokee kwa kuanza na neno ya “Lite Up My Weekend”. wateja watakaofanya vizuri watapata zawadi mbalimbali kila wiki. Alisema Makau.
Zaidi ya zawadi za kila wiki, wateja pia watashinda nafasi za kuhudhuria matamasha mbalimbali yanayoambatana na muziki hapa nchini. Ninawaomba sana wapenzi wa bia hii ya Castle Lite, kushiriki mara nyingi iwezekanavyo ili kushinda zawadi hizi za kuvutia, aliongeza Geoffrey.

MENINAH AKANUSHA UVUMI WA KUWA NA MAHUSIANO NA DIAMOND.


Stori ambayo Soudy Brown amei amplify kupitia You heard ya leo Aug 12 ni kuhusu uhusiano wa Diamond Platnumz na Meninah ambye inasemekana wanatoka kimapenzi, Soudy Brown kaongea na Meninah.

ANGALIA PICHA DIAMOND PLATINUMZ AFANYA KUFURU MWANZA...