Friday, August 31, 2012

WALIMU WAISHUKIA SERIKALI TENA

DAR ES SALAAM-TANZANIA,
http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2012/07/Gratian-Mukoba.jpgSerikali imedaiwa kupuuza amri ya  Mahakama iliyotakakuktana na Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ili kujadili maslahi ya walimu chini ya mshauri ambaye ni mtaalamu wa sheria za kazi.
Akiongea na waandishi wa habari hapo jana Rais wa chama cha walimu (CWT) Bw.Gratian Mkoba amesema licha ya agizo hilo la mahakama serikali haijawa tayari kukutana na walimu kusikiliza madai yao.

Mukoba kwa niaba ya CWT ameitaka serikali kukutana na walimu kabla ya Septemba 10, siku ambayo shule zinafunguliwa vinginievyo chama chake kitachukua hatua kitakazoona zinafaa.



Mukoba alisema Agosti 2, mwaka huu chama chake kilimwandikia Katibu Mkuu  Kiongozi barua yenye kumbu namba CWT/004/IKULU/VOL.1/48  nia yao ya kukutana naye kujadili madai hayo
ambapo aliwajibu atajadiliana na wenzake kuhusu suala hilo.
ukoba aliongeza kuwa agosti 6 waliandika tena barua ingawa haijapewa majibu mpaka sasa.

“Kitendo cha serikali kukaa kimya kwa muda wa siku 27 bila ya kuonesha kujali kutekeleza kwa amri ya mahakama kunatafsiriwa na CWT kama ni kukosekana kwa nia njema ya serikali kusikiliza madai ya walimu tofauti na propaganda zilizoendelezwa wakati wa mgomo juu ya utayari wao wa kujadiliana na walimu,” alinukuliwa Mukoba.

Mukoba aliitaka pia serikali kuwarudishia madaraka walimu iliowavua madaraka na kufuta mashitaka yote dhidi ya walimu inayodai walishiriki katika mgomo.Pia rais huyo ameitaka serikali kumaliza tatizo hilo mapema ili kuwapa matuamaini walimu kala ya shule kufunguliwa.

SHAMBULIO LA RISASI LAUA WATATU MAREKANI




NEW YORK-MAREKANI 
Mwanaume mmoja aliyetambulika kwa jina la Terence Tyler, (23) amewapiga na kuwaua wafanyakazi wanzake kwa risasi na kujiua mwenyewe katika duka la New Jersey wanapofanya kazi leo hii mjini nje kidogo ya Jiji la New York huko Marekani.Waliouawa wametambuliwa kuwa ni binti wa miaka 18, Cristina LoBrutto na kijana Bryan Breen mwenye umri wa miaka 24.

Terence ambaye aliwahi pia kuwa mwanajeshi wa jeshi la maji la Marekani alikuwa akifanya kazi katika duka hilo kwa muda unaokadiriwa kuwa wiki 2, na imedaiwa kuwa chanzo cha mauaji hayo ni kukosana na mmoja wa wafanyakazi wenzake.Polisi wamesema Terence alikwaruzana na mfanyakazi mwenzake leo asubuhi na akatoka na baadaye kurudi na bunduki pamoja na bastola ambapo aliwapiga risasi wafanyakazi wenzake wawili kabla ya kujipiga mwenyewe.

Wafanyakazi wenzake walifunga milango wakati akirudi ingawa alifanikiwa kuwapiga risasi kupitia dirishani.

Tukio hilo ambalo limetokea kabla ya kufunguliwa duka hilo, limekuwa ni mwendelezo wa matukio ya upiganaji risasi nchini humo baada ya lile lililotokea katika jumba la makumbusho la Sikh temple ambapo watu 6 waliuawa pamoja na lile lililotokea katika filamu ya Batman ambapo watu 12 waliuawa hali inayoongeza shinikizo juu ya sheria za uuzaji wa silaha nchini Marekani.