Friday, August 24, 2012

MTUHUMIWA WA MAUAJI YA NORWAY AFUNGWA MIAKA 21.


http://s1.reutersmedia.net/resources/r/?m=02&d=20120824&t=2&i=645573356&w=460&fh=&fw=&ll=&pl=&r=CBRE87N0N8A00

OSLO-NORWAY,
 Mahakama nchini Norway imemkuta na hatia na kumhukumu kifungo cha miaka 21 jela, mtuhumiwa wa mauaji ya watu 77 nchini Norway Bw.Anders Behring Breivik. Matuhumiwa huyo alidaiwa kuhusika na mauaji ya watu 77 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 240 wakati alipotega bomu katikati ya mji wa Oslo na baadae kuwapiga kwa risasi vijana waliokuwa katika kambi moja huko Camp Island.

Mtuhumiwa huyo alikiri kufanya makosa hayo na kukataa kuitwa mkosaji akitetea uamuzi wake kuwa ni sahihi kwa kuwa alikuwa akizuia kuenea Uislam Norway.Kesi hiyo ambayo imedumu kwa miezi kadhaa ilikuwa na mvutano ambapo licha ya kuonekana na hatia mawakili na serikali walikuwa na mvutano ikiwa mtuhumiwa huyo yupo timamu au ana matatizo ya akili hali iliyokuwa ikileta utata juu ya hukumu anayostahili, ingawa hatimaye serikali imajiridhisha kuwa mtuhumiwa huyo anastahili hukumu.

Hukumu hiyo imewekwa wazi ambapo itaweza kuongezwa kwa miaka zaidi ya 21 ikiwa mtuhumiwa huyo ataonekana bado ni hatari kwa jamii yake hata baada ya kumaliza kifungo chake.

Familia na ndugu wa Marehemu na waathirika wa tukio hilo wameridhishwa na hukumu hiyo,"Amepata anachostahili," alisema Alexandra Peltre, 18,ambaye alipigwa risasi na kujeruhiwa na mtuhumiwa huyo.Bi. Per Balch Soerensen,  ambaye binti yake aliuawa katika shambulio hilo alisema anashukuru hukumu hiyo imefika mwisho kwa sababu watakuwa na amani na utulivu tena.

Mtuhumiwa huyo akivalia sare kama za polisi alilipua bomu pamoja na kuwapiga risasi vijana waliokuwa katika kambi huko Norway, na kusababisha vifao vya watu 77 hapo mwezi Julai Mwaka jana.

MWAKYEMBE AMSIMAMISHA MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA BANDARI

DAR-ES-SALAAM-TANZANIA,
WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Bw.Ephraim Mgawe, Pamoja na wafanyakazi wengine wakiwemo wasaidizi wake wawili na meneja wa Bandari hiyo Bw.Cassian Ng'amilo kupisha uchunguzi wa tuhuma za uzembe, pamoja na wizi wa vitu mbali mbali yakiwemomafuta na  makontena yanayosafirishwa kupitia bandari hiyo.

Akizungumza baada ya hatua hiyo waziri Mwakyembe amesema bandari ya Dar es Salaam imekuwa ikikosa wateja ambao wameamua kusafirishia mizigo yao kupitia bandari za Msumbiji na Afrika Kusini kutokana na kukithiri kwa wizi katika bandari hiyo.Waziri huyo aliongeza kuwa serikali haiwezi kukaa na kukosa mapato kwa sababu ya wizi uliopita kiasi.

Waziri huyo pia ameunda kamati ya watu sita ingawa hakuwataja kwa majina ili kuchunguza wizi huo akiwapa maswali yenye hadidu za rejea zipatazo hamsini. Baada ya hatua hiyo Dk Mwakyembe amemteua Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira katika Wizara ya Ujenzi, Injinia Madeni Kipande kukaimu nafasi hiyo ya ukurugenzi wa bandari.Hatua hiyo imedaiwa kuchochewa na wizi wa makontena 40 ya vitenge yaliyokuwa yakisafirishwa nje ya nchi hivi karibuni.

Hiyo ni hatua nyingine kubwa kuchukuliwa na Waziri huyo ambaye Mwezi juni alimfukuza Kaimu mkurugenzi wa shirika la ndege la Tanzania(ATCL) Bw.Paul Chizi.

WANAMGODI WALIOUAWA AFRIKA KUSINI WAOMBEWA.

http://gdb.voanews.eu/D6665CE2-085E-4BB6-B650-D6E5CE826744_mw800_s.jpgJOHANNESBURG- AFRIKA KUSINI
  Maelfu ya ndugu,jamaa na marafiki wa marehemu waliofariki wiki iliyopita katika mapambano kati ya wachimba mgodi wa Marikana na polisi walikusanyika hapo jana katika ibada ya pamoja kuwaombea marehemu hao. Ibada hiyo imefanyika katika eneo yalipotokea mauaji hayo huko Marikana ambalo limepewa jina la "Uwanja wa mauaji wa Afrika Kusini" na wanamgodi hao.

Viongozi wa kidini na kijadi ndiyo walioongoza ibada hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na baadhi ya viongozi wa serikali na vyama vya wafanyakazi.Moja wa viongozi wa kidini alikuwa ni Daniel Modisenyane  aliwaambia waliohudhuria kuwa jamii itajitahidi kupambana na hasara hiyo.
" Siyo rahisi kwa wafiwa kusahau kwa kuwa limekuwa tukio la kuumiza na hatujui hata tutawatuliza vipi" Alisema Modisenyane.

Viongozi wengine waliilaumus serikali kwa kuhusika na mauaji hayo na kuitaka kuchukua hatua kali kwa waliohusika.
Misa hizo zilifanyika pia katika sehemu mbalimbali nchi nzima.