Wednesday, December 05, 2012

WAASI WAIZUNGUKA KAMBI YA VIKOSI VYA ANGA SYRIA-TISHIO LA ASSAD KUTIMUI SILAHA ZA SUMU LAONGEZEKA




Mzozo wa Syria
DAMASCUS-SYRIA,Waasi wameizingira kambi moja ya kikosi cha anga karibu na Damascus, wakati Marekani ikieelezea wasi wasi wake kwamba Rais Bashar al Assad wa Syria anayetapatapa huenda akatumia silaha za sumu kukabiliana na upinzani.
Clinton amesema leo hii kwamba Marekani ina wasi wasi kuwa Rais Bashar al Assad wa Syria ambaye anazidi kutapatapa anaweza kuamuwa kutumia silaha za sumu au kupoteza udhibiti wake kwa silaha hizo.Baada ya kukutana na mawaziri wa mambo ya nje wa Jumuiya ya NATO mjini Brussels Ubelgiji ambapo jumuiya hiyo ya kijeshi ya mataifa ya magharibi imekubali kupeleka Uturuki nchi jirani na Syria makombora ya kujihami ya patriot ambapo hutumika kudukiza makombora yanayorushwa kutoka nje, Clinton amesema serikali ya Marekani imeweka wazi kwa Syria kwamba Marekani itabidi kuchukuwa hatua iwapo nchi hiyo itatumia silaha za sumu.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Hillary Clinton.Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Hillary Clinton.
Clinton ameuambia mkutano wa waandishi wa habari mjini Brussels kwamba wasi wasi wao Assad anayezidi kutapa huenda akaamuwa kutumia silaha za sumu au akapoteza udhibiti wa silaha hizo kwa mojawapo ya makundi mengi ambayo hivi sasa yanaendesha harakati zake nchini humo.Waasi nchini Syria wamesema leo hii kwamba wameizingira kambi moja ya kikosi cha anga karibu na mji mkuu wa Damascus ikiwa ni ishara mpya kwamba mapigano hayo hayo yanazidi kuunyemelea mji mkuu huo.
Mapigano yapamba moto
Mapigano makali yamezuka karibu na mji wa Damascus wiki moja iliopita na kuvikisha vita hivvyo kwenye kitovu cha utawala wa Assad ambapo huko nyuma vilikuwa vikipiganwa kwenye majimbo. Wapiganaji wamesema wameizunguka kambi ya kikosi cha anga ya Aqraba ilioko kama kilomita 4 nje ya mji mkuu.Abu Nidal msemaji wa kikosi cha wapiganaji waasi cha Habib al Mustafa amesema wanataraji kuiteka kambi hiyo masaa machache yajayo.Ameongeza kusema kwamba waasi wamekiteka kituo cha wanajeshi wa anga kilioko karibu na hapo na kimeuwa wanajeshi kadhaa,kuwatia nguvuni wengine na wengine kadhaa wameweza kukimbia.Habari kama hizo kutoka Syria imekuwa vigumu kuzithibitisha kutokana na serikali kuzuwiya vyombo vya habari kurepoti nchini humo.
 Mojawapo ya viunga vya Damascus vilivyoshambuliwa na ndege za Assad.Mojawapo ya viunga vya Damascus vilivyoshambuliwa na ndege za Assad.
Mkakati wa wanajeshi ni kuigawa Damascus makao makuu ya utawala wa Assad kutoka viunga vilioko nje ya mji huo ambapo waasi wamekuwa wakizidi kuvidhibiti. Mashambulizi ya anga yamekuwa yakiendelea kwa zaidi ya wiki moja dhidi ya viunga hivyo ambapo wanaharakati wanasema ni mashambulizi makubwa kuwahi kushuhudiwa kwenye viunga hivyo.
Duru za serikali ya Syria zimesema jeshi limeweza kuwarudisha nyuma waasi kwa kilomita 9 kutoka mji mkuu. Waasi hawakuthibitisha wala kukanusha habari hizo lakini wamesema lengo lao haliko katika kuingia wenye mji huo kwa sasa.
Makobombora ya Kujihami kwa Uturuki
Aina ya makombora ya Patriot yatakayowekwa katika mpaka wa Uturuki na Syaria.Aina ya makombora ya "Patriot " yatakayowekwa katika mpaka wa Uturuki na Syaria.
Kwa upande mwengine uamuzi wa NATO wa kutuma makombora ya kujihami ya Marekani, Ujerumani na Uholanzi kusaidia kuulinda mpaka wa Uturuki utavifikisha vikosi vya Marekani na Ulaya kwenye mpaka wa Uturuki kwa mara ya kwanza kabisa katika mzozo huo wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Syria viliodumu kwa miezi 20 sasa.
NATO imesema makombora hayo inayoyatuma Uturuki ni kwa ajili tu ya kujihami lakini Syria na washirika wake wa Urusi na Iran wameushutumu uamuzi huo kwa kusema kwamba unazidisha hali ya ukosefu wa utulivu katika eneo hilo.

KUELEKEA UCHAGUZI KENYA-Mudavadi ajiunga kambi ya Ruto na Uhuru, huku Odinga, Musyoka, Wetangula na Ngilu waunda kambi yao



Waziri mkuu Raila Odinga na makamu wa rais Kalonzo Musyoka wakitia saini muungano wa vyama vyao vya ODM/WIPER/FORD-K/NARC
Waziri mkuu Raila Odinga na makamu wa rais Kalonzo Musyoka wakitia saini muungano wa vyama vyao vya ODM/WIPER/FORD-K/NARC
RFI
















NAIROBI-KENYA, Harakati za kisiasa nchini Kenya zimeendelea kushika hatamu kufuatia wagombea mbalimbali wanaowania urais kutangaza miungano yao na vyama vingine kwa lengo la kuhakikisha wanapata ushindi kwenye uchaguzi mkuu wa hapo mwakani.

Muungano wa kwanza ulikuwa ni ule wa vyama vya URP cha mbunge wa Eldoret kaskazini William Ruto na mwenzake wa TNA ambaye pia ni naibu waziri mkuu Uhuru Kenyatta kutiliana saini siku ya Jumapili.
Tarahe 4 ya mwezi huu ndio ilikuwa siku ya mwisho kwa vyama mbalimbali kutangaza miungano yao ambapo waziri mkuu Raila Odinga na chama chake cha ODM kilitangaza kuungana na chama cha Wiper cha makamu wa rais Kalonzo Musyoka na kile cha FORD-K cha Moses Wetangula.
Kuungana kwa waziri mkuu raila Odinga na makamu wa rais Kalonzo Musyoka kulitabiriwa na wachambuzi wa masuala ya siasa ambao walisema kutokana na viongozi hao kuungana mwaka 2002 chini ya mwavuli wa NARC kulikuwa na uwezekano mkubwa pia kwa mwaka huu kuungana kwaajili ya uchaguzi ujao na sasa watakuwa chini ya mwavuli wa CORD.
Katika muungano wao mbali na kuwepo kwa chama cha FORD-K Moses Wetangula, pia mwenyekiti wa chama cha NARC Charity Ngilu alitangaza kujiunga kwenye muungano huo ambao sasa unajumuisha vyam 14.
Viongozi wote kwa pamoja wameapa kuwaunganisha wakenya na kuijenga kenya bora isiyo na migogoro ya kidini wala kikabila kama ilivyojitokeza kwenye uchaguzi wa mwaka 2007/2008.
Katika hatua nyingine naibu waziri mkuu Musalia Mudavadi wa chama cha UDF alitangaza kuungana na William Ruto na Uhuru Kenyatta katika mbio za kuwania kuingia ikulu mwaka 2013.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaona kuwa licha ya kuwepo miungano ya vyama mbalimbali bado viongozi hao wanachangamoto kubwa ya kuhakikisha wanaondoa ukabila ambao baadhi ya wagombea wametuhumiwa kujiunga kutokana na maeneo wanayotoka.
Muungano wa CORD kati ya Raila Odinga na Kalonzo Musyoka bado wenyewe hawajatangaza ni nani atakayewania kiti cha urais na jambo hilo litaamuliwa kwenye mkutano mkuu wa vyama vyao.(CHANZO RFI)