Tuesday, June 10, 2014

SOMA ALICHOSEMA PROF J BAADA YA DIAMOND KUKOSA TUZO

Msanii mkongwe wa Hip Hop Proffesor Jay amesema kuwa kushindwa kwa Diamond kuchukuwa tuzo za MTV kusimvunje moyo kwakuwa alikuwa anashindana na wasanii wakubwa sana Africa.

Akizungumza na mtandao huu leo ,Proffesor Jay amesema kuwa nafasi aliyopata Diamond na kushindana na wasanii hayo ni ushindi mkubwa wake.
“Diamond lazima ajue katika mashindano kuna kushinda na kushindwa, Kitu ambacho ninaweza kumwambia Diamond asikate tamaa, ameshindanishwa na wasanii wakubwa sana ambao pia ni advantage kwake ,msanii kama Davido pamoja na kufanya muziki mzuri tutambue kuwa nyuma yake kuna Wanageria zaidi ya milioni 150, ambao kiukweli wenzetu wameamka sana kuchangia kuwa support wasanii wao, sisi Watanzania tumekuwa tunazungumza kwa maneno mengi kulipo vitendo ,so mtu kama Davido ameshinda kwa kupigiwa kura na watu wake wengi na muziki wake umefika afrika nzima. Kwaiyo kushindwa kwake Diamond asichukulie kukata tamaa ,yeye achukulie kama changamoto na kuwashawishi Watanzania na mashabiki wake kuendelea ku support muziki wake ili afike mbali zaidi, naamini kuna kila dalili kwa Diamond kuendelea kufanya vizuri zaidi hapo mbeleni, pia nataka niwaambie Watanzania kwamba mtu anapoiwakilisha Tanzania tujitaidi kuweka tofauti zetu nyuma na kum,support wasanii wetu kwa sababu ushindi wake ni mafanikio makubwa ya muziki wetu,wasanii na wetu, na taifa kwa ujumla” Alisema Proffesor Jay.

Katika hatua nyingine Proffesor Jay amesema kuwa kesho anaingia mzigoni kuanza kushoot video ya ‘Kipi Sijasikia’ “Kesho naanza ku,shoot video ya Kipi Sijasikia, kilichotokea nilikuwa namsubiri tu Diamond, kwa sababu ratiba yake ilikuwa imebana sana, kila kitu sasa hivi kipo set, na tunafanya na Adam Juma, kilichotufanya tu delay kidogo ni kwa sababu alikuwa ameagiza Red na vitu vingine, kwaiyo vikawa vimechelewa kidogo lakini baada ya kuingia vyombo vyake, kesho tunaanza lakini ataujajua tutamaliza lini.Adam amenivutia sana sasa hivi kwa sababu ya kubadilisha kamera , Adam ana skills kubwa ya kutumia kamera , lakini kamera ambazo alikuwa akitumia mwanzo zilikuwa zinambana kidogo lakini sasa hivi kwa kuleta kamera hiyo Red na vitu vingine kama hivyo tunategemea uwezo wake anaweza akaonyesha kwa mapana zaidi , na pia tumejaribu tunatumia advantage ya Diamond huko anakozunguka kujaribu kufanya connection, kwa sababu Diamond anaweza kusaidia muziki wetu kifika mbali zaidi”Alisema Proffesor.

MWANAMKE ALIYEFANYA MAPENZI NA SAMAKI AINA YA DOLPHIN AONGEA KWA MARA YA KWANZA.

mager
Unaweza kushangaa na kuona ni kitu cha ajabu lakini hii imetokea ambapo mwanamke ambaye alifanya mapenzi na samaki aina ya Dolphin ikiwa ni sehemu ya utafiti wa kisayansi amezungumza kwa mara ya kwanza juu ya hatua hiyo.
Mwanamke huyo Margaret Howe Lovatt ambaye ni mtafiti wa wanyama amesema alikuwa sehemu ya utafiti huo uliofanyika katika kisiwa cha Virgin nchini Marekani kwa ajili ya kuwafundisha viumbe wa baharini wenye akili jinsi ya kuongea kiingereza.
Margaret Lovatt Howe
Margaret Howe Lovatt anasema alikuwa akijaribu kumfundisha Peter (the dolphin) jinsi ya kuongea kiingereza lakini uhusiano wao ulikwenda mbali zaidi.
Ilikuwa mnano wa mwaka 1963 ambapo walimsaidia kutengeneza bwawa la Dolphin nyumbani kwake ambako wanasayansi wangeweza kuwasoma wanyama hao wakiwa nyumbani, ndipo hapo Margaret alipokuna na Peter ambaye ni samaki aina ya Dolphin kwa wakati huo akiwa bado mdogo ambapo wawili hao wakapatana na mahusiano yao kukua zaidi kimwili.
Margaret amenukuliwa akisema kuwa “Peter (Dolphin) alipenda kuwa na mimi, mara nyingi alikuwa akijisogeza mwenyewe karibu yangu kwenye mguu wangu au mkono na kuruhusu kitendo hicho.”
dolphin
Anaendelea kusema kuwa “Haikuwa shida kwangu kwani Peter alikuwa akihisi uwepo wangu na kuona ni kitendo cha kimapenzi kwa upande wake lakini kwangu niliona ni kitu cha kawaida kama sehemu ya masomo yangu.”