Saturday, February 02, 2013

CLINTON AJIUZURU RASMI,ADAIWA KUTAKA KUGOMBEA URAIS 2016

U.S. Secretary of State Hillary Clinton shakes hands with Deputy Secretary of State Thomas Nides as she bids farewell on her last day in office at the State Department in Washington February 1, 2013.  REUTERS/Kevin Lamarque  (UNITED STATES - Tags: POLITICS)


WASHINGTON-MAREKANI,
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bi. Hillary Rodham Clinton amejiuzuru rasmi hapo Ijumaa ya jana akimaliza miaka mine ya kulitumikia taifa hilo kama waziri wa ulinzi.Katika barua yake kwa rais Obama waziri huyo amemshukuru rais huyo kwa kumpa nafasi ya kutumikia katika utawala wake akisema nafasi hiyo imempa heshima.
"Ninaamini katika uongozi wa Marekani katika ulimwengu kama nguvu katika kuleta ulimwengu bora" alisema Bi.Clinton.
Kujiuzuru kwa waziri huyo kumeanza baada ya kuapishwa kwa John Kerry jana hiyo.
 
Licha ya kuwa kujizuru huko ni kwa kawaida Bi,Clinton ameacha lawama kwa uongozi wa rais Obama kutokana na kuonekana kutowajibika kuzuia shambulio la ubalozi wa Marekani hapo Septemba mwaka jana ambapo lilimuua balozi wa Marekani nchini humo.Ingawa kwa upande wake Bi.Clinton amekuwa akishindwa kukubali moja kwa moja kuwajibika huko akisema hakuna ushahidi dhahiri wa kuonesha kushindwa au kuzembea kwake katika tukio hilo.
 
Katika hatua nyingine kumekuwepo na tetesi za mama huyo kugombea urais hapo mwaka 2016, huku Bi.Clinton akisema kwa sasa anaenda kupumzika na atafikiria kuhusu uamuzi huo ingawa amesema tukio la Benghazi halitoathiri uamuzi wake wa kugombea Urais mwaka 2016.(YAHOO NEWS)

SERIKALI YABANWA MJADALA WA KUBADILI MTAALA WA ELIMU BUNGENI


DODOMA-TANZANIA,
HOJA binafsi ya mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia, imeibua mapya bungeni mjini Dodoma, baada ya Kambi ya Upinzani kukutana kwa dharura, kupinga kufifishwa hoja hiyo na Naibu Spika, Job Ndugai, wakidai anataka kuizima.


Juzi Mbatia aliwasilisha bungeni Hoja Binafsi kuhusu udhaifu wa elimu Tanzania, akitaka mfumo mzima unaosimamia elimu nchini ufumuliwe.
Baada ya majadiliano marefu kuhusu kuundwa kwa kamati ya kuchunguza mitalaa, sera na
mihutasari ya elimu, hoja mbalimbali zilitolewa, baadhi ya wabunge wakitaka Kamati ya Bunge, huku wengine wakitaka iundwe tume huru ya kufuatilia suala hilo.


Mjadala huo uliendelea jana asubuhi kwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa kusimama na kutetea mfumo wa elimu uliopo na mtalaa, kabla ya wabunge kuchangia na Mbatia kuhitimisha.


Akiwasilisha hoja yake, Mbatia aling’ang’ania kupatiwa mtalaa wa masomo ya elimu kwa shule za msingi na sekondari, jambo ambalo, Waziri Kawamba alijibu kuwa ulikuwapo ingawa hakuwa nao bungeni.
Baada ya majibu ya Dk Kawambwa, Mbatia aliomba hoja yake iahirishwe hadi mtalaa utakapowasilishwa bungeni.


Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi alisimama na kusema akihoji: “Katika kikao kilichopita, hata katika Hansard, tulisema mtalaa utawasilishwa katika kikao hiki, sasa wasiwasi wa mbunge (Mbatia) ni nini? Hata siku ya mwisho ya Bunge tutaleta.”


Baada ya kauli hiyo, Naibu Spika, Job Ndugai alipiga kura kwa kuuliza wanaotaka hoja imalizike na baada ya majibu, aliruhusu Mbunge wa Nzega, Dk Hamis Kigwangalla kuwasilisha Hoja Binafsi kuhusu ajira kwa vijana na kilimo.


Hata hivyo, baada ya kumruhusu Dk Kigwangalla, wabunge wa upinzani walitoka nje ya Bunge na kufanya mkutano wa dharura uliochukua dakika 38 katika Ukumbi wa Pius Msekwa.


Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa kikao hicho, Tundu Lissu aliwaeleza sababu za wao kutoka nje ya Bunge na hatua za kuchukua.


“Tumewaita kuzungumzia sababu za kutoka nje na hatua za kuchukua. Kama mlivyosikia, Mbatia alisema kuwa hakuna mitalaa wala hakujawahi kuwa na mitalaa tangu mwaka 1961 na kama ipo atajiuzulu. Alipomtaka Waziri ampe japo nakala, waziri alikataa,” alisema Lissu na kuongeza:


“Sasa tunachosema ni kwamba, Waziri Kawambwa amelidanganya Bunge na tutapeleka taarifa ya kikao chetu katika Kamati ya Bunge ya Mamlaka ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge, kumtaka ajiuzulu kwa kulidanganya Bunge, ikishindikana tutapeleka kwa Mamlaka zilizomteua.”
Alisisitiza: “Na hapa ikishindikana pia kumwajibisha, tutapiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu.”
Hata hivyo, Lissu akiwa pamoja na Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema na Mbatia meza kuu, alisema kuwa tangu kuanza kwa vikao vya Bunge, Spika Anne Makinda na naibu wake Ndugai, wameonyesha nia ya kufifisha hoja za upinzani.


Alisema: “Tulitaka kujadili hoja ya suala la gesi ya Mtwara, lakini Spika akazima, akasema itaundwa tume, baadaye akasema tume hakuna baada ya Waziri Mkuu kwenda, tangu Mbatia kuwasilisha hoja yake, inaonekana waziwazi wanataka kuizima.”


Lissu aliongeza: “Kanuni ziko wazi, maspika wamekula kiapo kufanya kazi bila upendeleo, lakini hapa hawatendi haki, sasa sisi kama Kambi ya Upinzani, vilevile tutaandaa hoja kwa lengo la kumwondoa spika na naibu wake.”(MWANANCHI)