Monday, August 06, 2012

WAZIRI MKUU WA SYRIA AJIUNGA NA UPINZANI

http://www.aljazeera.com/mritems/Images/2012/8/6//201286101153313734_20.jpg
Waziri mkuu aliyejiuzuru Bw.Hijab alipokuwa akiapishwa na Rais Al-Assad.

DAMASCUS-SYRIA
Waziri mkuu wa Syria Bw.Riad Farid Hijab, amejiunga na upinzani baada ya kutangazwa kufukuzwa wadhifa wake huo leo asubuhi.Waziri huyo mkuu ameripotiwa kuwasili Jordan leo na kutangaza kujiunga na upinzani,
"Natangaza kuanzia leo kuondoka katika mkondo wa kigaidi na mauaji na kuanzia leo mimi ni mwanajeshi niliyebarikiwa na ninajiunga na kundi la wanamapinduzi na wapigania uhuru" alinukuliwa Hijab katika taarifa yake iliyosomwa na msemaji wake Muhammad el-Etri.
 .
Etri alikanusha pia kuwa waziri mkuu huyo amefukuzwa akisema kuwa serikali imetoa tangazo la kumfukuza baada ya kutambua ameshaondoka nchini Syria.Etri amesema pia kuwa Hijab alikuwa na mpango huo na alikuwa akiwasiliana na jeshi la waasi la Free Syrian Army.

Katika taarifa yake hiyo waziri mkuu huyo mstaafu amewataka viongozi wengine wa Syria kuondoka na kuachana na serikali ya Bw.Al-Assad.
Bila shaka hilo litakuwa ni pigo kubwa kwa Rais Al-Assad ambaye mwezi uliopita aliwapoteza mawaziri wawili katika shambulio la bomu nchini humo.

USAIN BOLT ASHINDA TENA MEDALI YA DHAHABU.

http://www.abc.net.au/news/image/4178898-3x2-700x467.jpgLONDON-UINGEREZA,
Usain Bolt mwanariadha mwenye kasi zaidi duniani ameonesha umahiri wake baada ya hapo jana kunyakua medali ya dhahabu akishika nafasi ya kwanza katika mbio za mita 100 wanaume, huku akiweka rekodi mpya ya kukimbia mita 100 kwa sekunde 9.63.
 Nafasi ya pili ilienda kwa mjamaika mwenzake Yohan Blake na ya tatu  ikachukuliwa na bingwa wa mbio hizo mwaka 2004 Justin Gatlinwa Marekani.
http://jahkno.com/wp-content/uploads/2012/08/Usain-Bolt-The-Legend-Wins-100m-London-2012-Olympic-111.jpg
 Ushindi huo wa Bolt umedhihirisha ubora wake na utawala katika riadha na kuwaondoa hofu mashabiki wake ambao walihofu angeshindwa kutokana na kuripotiwa kuwa na majeraha ya mkono.Wajamaika ambao hapo jana walikuwa pia wakisheherekea uhuru wa nchi yao wameupokea kwa shangwe ushindi huo.
Bolt sasa atalingana na mwanamichezo Carl Lewis wa Marekani ambaye naye amewahi kupata medali 2 za dhahabu katika mbio hizo za mita 100.


Wajamaica wakishangilia Ushindi huo katika jiji la kingstone -Jamaica.

"Baada ya nusu fainali nilipata ujasiri na kujiamini kwani miguu yangu ilikuwa vizuri na hicho kiliniongezea kujiamini" alisema Bolt baada ya ushindi huo.