Sunday, February 12, 2012

WHITNEY HOUSTON AFARIKI!!

Whitney Houston, Mwanamuziki mkongwe na maarufu wa muziki wa Pop/RnB ambaye alishawahi kufikia kiwango cha mauzo ya Multiplatinum katika album zake za miaka ya 1980 kuelekea 1990, na kuchaguliwa kuwa moja ya wanamuziki wa kike mwenye mafanikio zaidi katika muziki wa Pop duniani, amefariki dunia siku ya jumamosi iliyopita akiwa na umri wa miaka 48.





Whitney Elizabeth Houston - aliyezaliwa mwezi August 9, 1963 amekutwa akiwa amefariki katika Hoteli ya Beverly Hillton na kwa mujibu wa polisi wa Beverly Hills wamesema Whitney hakuna dalili za kuwepo kwa tukio la kihalifu lililosababisha kifo hicho ingawa pia chanzo cha kifo hicho hakijafahamika.


Whitney ambaye hivi karibuni alianza kurudi jukwaani tangu mwaka 2006 alipotalakiana na mumewe Bobby Brown baada ya ndoa yao ya miaka 14, wakiwa na mtoto wao Bobbi Kristina ,ambapo alifanikiwa kufanya wimbo mmoja na mwanamuziki Akon uliotambulika kwa jina la "Like I never Left" na katika siku za hivi karibuni kabisa akipata mwaliko wa kutumbuiza katika tamasha la utangulizi la utoaji wa uzo za Grammy kwa mwaka 2012 ingawa katika mazoezi sauti yake ilionekana kuwa dhaifu na isiyo na makali ya miaka ile tena.











Katika mafanikio yake whitney alivuma kama mwanamuziki bora wa kike duniani huku album zake zikishika chati za juu na kumuwezesha kuwa moja ya wasanii waliowahi kuuza zaidi duniani. Pia Whitney amewahi kuvuma katika anga za filamu ambapo alicheza katika filamu za "The Bodyguard" na "Waiting to Exhale" huku nyimbo zake zikitumika kama soundtracks na kumpatia mauzo ya kiwango cha juu.





Akiwa Binti mdogo Whitney mtoto wa muimbaji wa nyimbo za dini Cissy Houston na marehemu John Houston aligunduliwa kipaji chake na clive Davis aliyekuwa Producer katika lebo ya Arista Records mwanzoni mwa miaka ya 1980 ambaye alimuongoza kuuza jumla ya nakala milioni 170 za sauti na video huku nyimbo zake za "I will always love you" na " The Greatest Love of All".


Hata hivyo maisha ya mwanamuziki huyo baadae yalitawaliwa na matumizi ya pombe na dawa za kulevya hali iliyomuathiri afya yake.








Pamoja na yote Whitney Houston atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika muziki ambao umewaathiri vizazi vya sasa wakiwemo wanamuziki Brandy, Monica, Mariah Carey, Beyonce na Christina Aguilera ambao wameiga mfano wake, pia atakumbukwa kwa kujishighulisha na masuala ya kijamii ikwemo haki za wamarekani weusi hasa katika masuala ya Elimu.









MwenyeziMungu mwenye Rehema ailaze mahali Pema Peponi roho ya mpendwa wetu Whitney Houston Amen!




LA LIGA:BARCELONA WABANWA NA OSASUNA

Wachezaji wa Barcelona wakiwa na huzuni hapo jana mara baada ya Kupoeza dhidi ya Osasuna.


Hispania,
dejan lekic hapo jana aliisaidia timu yake ya Osasuna kuiangusha moja ya miamba ya soka Nchini Hispania Barcelona kwa jumla ya magoli 3-2.
Osasuna walipata goli lao la kwanza kupitia kwa mchezaji huyo Dejan katika dakika ya sita ya kipindi cha kwanza.Dakika 16 baadae katika dakika ya 22 Osasuna waliongeza goli lao la pili kupitia kwa mchezaji yule yule Dejan na kuwafanya waende mapumziko wakiongoza kwa magoli 2-0.
Baada ya mapumziko kocha wa Barcelona alifanya mabailiko na kumuingiza Kapteni Carles Puyol abaye aliongeza nguvu na kuwafanya Barcelona kupata goli katika dakika ya 6 ya kipindi cha pili kupitia kwa Alexis ssanchez ingawa furaha hiyo haikudumu kwani dakika ya 73 mchezaji Raul Garcia aliiandikia timu yake goli la tatu.
Zikiwa zimebaki dakika chini ya 20 mchezo kumalizika barcelona waliongeza bidii na kufanikiwa kupata goli la pili baada ya Cesc Fabregas kumtumbukizia Mpira Christian Tello ambaye hakufanya ajizi na kufunga goli hilo.

Baada ya goli hilo matokeo yalibaki hivyo mpaka mwisho wa mchezo na kuwafanya Barcelona wakizidi kuachwa katika msimamo wa ligi hiyo na Mahasimu wa Real Madrid kwa Point saba huku Madrid bado wakiwa na mchezo mkononi.

CHELSEA HOI KWA EVERTON- yafungwa 2-0, Pienaar awa mwiba.


Mchezaji wa afrika Kusini Steven Pienaar alikuwa mwiba mkali Everton ilipoichapa Chelsea Kwa magoli 2-0, akifunga goli la kwanza huku lile a pili likifungwa na Muagentina denis Stracqualursi katika kipindi cha pili.
Evertonambao hapo jana walikuwa wenyeji katika uwanja wao wa Goodison Park walianza kwa kasi na kufanikiwa kuapata goli lao la kwanza katika dakika ya 5 baada ya mpira uliomgonga Frank lampard Kumkuta Pienaar ambaye alipiga shuti kali la karibu lililomshinda kipa Petr Cech.

Everton nusura wapate goli la pili katika dakika ya 18 wakati Petr Cech aliposhindwa kuondoa mpira katika hatari na kumkuta Landon Donovan nje kidogo ya kumi na nane amabapo hata hivyo shuti lake hafifu liliokolewa na kipa huyo.
Chelsea nao walijitahidi kuongeza nguvu katikati mwa kipindi cha kwanza ambapo walikaribia kupata goli katika nafasi mbili ya kwanza katika dakika ya 25 ambapo shuti la michael Essien liliokolewa na Mlinzi wa Everton na lile lililofuatia la daniel Sturridge liliokolewa pia, huku nafasi nyingine ya Juan Mata ambaye alipiga shuti baada ya kupokea mpira kutoka kwa Sturridge ndani ya Eneo la penati liliishia kumgonga mlinzi wa Everton na kuwa Kona.

Hata hivyo chelsea walishindwa kuendeleza mikiki mikiki hiyo katika kipindi cha pili na kujikuta wakifungwa goli la pili dakika ya 72 katika kipindi cha pili baada ya Neville kumnyang'anya mpira Ashley Cole na Kumkuta Laandon Donovan ambaye alipiga shuti kali lililompita Petr cech licha ya kulipangua na kutua wavuni.

Licha ya kupigana zaidi Chelsea walishindwa kubadilisha matokeo na hadi mwisho wa mchezo matokeo yalibaki kuwa 2-0,na kuwafanya wenyeji hao wa Stamford bridge wakishindwa kuondoka na Point tatu katika mechi nne mfululizo.

ARSENAL WAIBURUZA SUNDERLAND-


Thiery Henry ameipatia ushindi mwingine Arsenal hapo jana ilipocheza na Sunderland, na kuifanya timu kushinda kwa jumla ya magoli 2-1 baada ya kutanguliwa kwa goli moja na Sunderland katika uwanja wa Light.

Dakika 45 za kipindi cha kwanza zilishuhudia Arsenal ikifanya mashambulizi machache kutokana na ulinzi imara wa Sunderland ingawa Arsenal walionekana kutawala kiasi kipindi hicho wakitumia nguvu za ziada kuwapita viungo na mabeki wa Sunderland.

Kipindi cha Pili kilianza kwa Arsenal kufanya mashambulizi ingawa bado awakufua dafu kwa safu ya ulinzi ya sunderland. Badala yake Sunderland ndio walioanza kufanya mashaambulizi kupitia kwa Craig Gardner katika dakika za 61na 63 na kumfanya kipa wa Arsenal Wojciech kufanya kazi ya ziada.
hatiimaye Sunderland walipata goli lao dakika ya 70 baada ya makosa ya mlinzi wa Arsenal ambaye alipoteza mpira na kumfanya james Mc Clean kufunga goli hilo.

Baada ya goli hilo Arsenal nao walikuja juu na kufanikiwa kusawazisha goli hilo katika dakika ya 75 kupitia kwa machezaji Aaron Ramsey aliyepiga shuti lililogonga mwamba na kuingia golini.

Na mwishowe matokeo yakiwa yanaonekana kuwa sare Mchezaji anayeshika vichwa vya habari tangu arudi tena kwa muda Arsenal mkongwe thiery Henry alifunga Goli katika dakika ya 91 ya ambao ulikuwa ni muda wa nyongeza akiunganisha krosi ya Andrei Arshavin na kuifanya Arsenal kuibuka na Ushindi wa magoli 2-1.

Thiery Henry ambaye amerudi Arsenal kwa muda kutoka Marekani ambako anacheza soka kwa sasa amekuwa chachu na msaada wa ushindi wa Arsenal katika siku za hivi karibuni na pengine timu hiyo inauwezekano wa kufikiaria kumrudisha katika kikosi hicho cha Arsene wenger.