Thursday, March 07, 2013

UCHAGUZI KENYA: RAILA ODINGA ATAKA KUSIMAMISHWA ZOEZI LA KUHESABU KURA.



NAIROBI-KENYA

Mgombea mweza wa Waziri Mkuu Raila Odinga, na Makamu wa Rais anayemaliza muda wake Kalonzo Musyoka ametoa wito kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya nchini Kenya IEBC kusitisha zoezi la kuhesabu kura za Urais baada ya kubainika kwa kasoro katika baadhi ya maeneo.


,Musyoka kutoka muungano wa kisiasa wa CORD amesema wana uthibitisho kuwa kumekuwa na udanganyifu katika zoezi hilo kwani katika baadhi ya maeneo kura za jumla zimekuwa zikizidi idadi ya wapiga kura waliojisajili hapo awali.
Licha ya kutoa kauli hiyo, Musyoka amewataka wananchi wa Kenya kuwa watulivu wakati huu kwani tuhuma hizo alizozitoa hazina lengo la kuhimiza maandamano ama vurugu kwani muungano wao unajiendesha kwa misingi ya sheria.

Maswali kadhaa yameendelea kuibuka baada ya mfumo wa uhesabuji kura wa kielekroniki wa IEBC kupata hitilafu na kulazimika zoezi la uhesabuji wa kura kuanza upya kwa njia ya kawaida.
Wakati hayo yanajiri IEBC imekuwa ikiendelea na uhesabuji wa kura hizo za Urais na imesema itatoa matokeo ya mwisho ifikapo siku ya Ijumaa asubuhi.
Licha ya IEBC kushindwa kutoa matokeo ndani ya saa arobaini na nane kama ilivyoahidi hapo awali kumekuwa na utulivu wakati wananchi wakiendelea kusubiri kinachoendelea kutoka Ukumbi wa Bomas jijini Nairobi ambapo matokeo rasmi yanaendelea kutolewa.
Kwa matokeo ya hivi sasa mgombea urais kwa tiketi ya muungano wa Jubilee Uhuru Kenyatta anaongoza akifuatiwa na Waziri Mkuu Raila Odinga ambaye ni mgombea wa muungano wa CORD.

MWENYEKITI WA JUKWAA LA WAHARIRI "ABSALOM KIBANDA" APELEKWA AFRIKA KUSINI KWA MATIBABU









Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahahariri na Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari 2006 Ltd,Absalon Kibanda akipakiwa kwenye ndege ya Kampuni ya Flightlink tayari kwa safari ya kwenda nchini Afrika Kusini kwa Matibabu baada ya kuvamiwa usiku wa kuamkia leo na watu wasiojulikana na kujeruhiwa vibaya,alipokuwa akirudi nyumbani kwake Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.

MWILI WA RAIS HUGO CHAVEZ WAAGWA-KUZIKWA IJUMAA

Mwili wa Marehemu Hugo Chavez katika gari.






Maelfu ya raia wa Venezuela wakiusindikiza mwili wa aliyekuwa rais wao.






Mwili wa Chavez umelazwa katika kituo cha mafunzo ya kijeshi mjini Caracas na marais wa nchi jirani walifika kutoa heshima zao za mwisho akiwemo Rais wa Bolivia Evo Morales na mwenzake wa Argentina Cristina Fernandez de Kirchner.
Add caption




Mwili wa aliyekuwa rais wa VEnezuela Bw. Hugo Chavez, Umepitishwa kwenye umati mkubwa wa wafuasi wake katika mitaa ya mji mkuu Caracas kuagwa na wafuasi na wananchi wa nchi hiyo.Kwa sasa  mwili huo umelazwa katika kituo cha mafunzo ya jeshi katika mji mkuu Caracas.
Watu wengi waliangua kilio huku wakichukua picha za kiongozi wao aliyefariki dunia .Mama yake na watoto wake walikusanyika mbele ya jeneza kutoa heshma zao .
Katika shughuli hiyo iliyoongozwa na makamu wa rais wa nchi hiyo Bw.Nicolas Maduro.


Mwili wa rais Chavez umepelekwa katika chuo cha kitaifa cha mafunzo ya kijeshi ambapo utazikwa kesho Ijumaa.
Bwana Chavez alifariki akiwa umri wa miaka 58 baada ya kuugua Saratani kwa zaidi ya miaka miwili.
Maelfu ya watu awali walikwenda barabarani mjini Caracas kutoa heshima zao za mwisho kwa Chavez wakifuatana na gari lililokuwa limebeba jeneza lake kuelekea katika chuo cha mafuzno ya jeshi.
Mazishi ya kitaifa ya Chavez yatafanyika Ijumaa.
Mkuu wa ulinzi wa Rais alinukuliwa akisema kuwa alikuwa na bwana Chavez alipofariki.
Generali Jose Ornella, alisema kuwa Chavez alifariki kutokana na mshtuko wa moyo na katika siku zake za mwisho kabla ya kifo cha ealisema angependa kuendelea kuishi.
Jeneza lake lililokuwa limefunikwa bendera ya nchi hiyo uliwekwa katika ukumbi ambao ni kumbukumbu ya waliopigania uhuru wa watu wa Amerika ya Kusini
Maelfu ya watu walipanga foleni kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu Chavez, wakiwemo maafisa wa serikali na viongozi wa Amerika ya Kusini,kama Rais wa Bolivia Evo Morales na Rais wa Argentina Cristina Fernandez de Kirchner.