Monday, April 23, 2012

Mgomo wa madaktari- Kikwete Aingilia Kati.

Kikwete aingilia kati mgomo wa madaktari

KIPANYA NA KUNJI LA MADAKTARI!

UCHAGUZI SENEGAL KUINGIA DURU YA PILI



DAKAR, SENEGAL,
                               Ikiwa Zaidi ya nusu ya kura zilizopigwa katika uchaguzi wa kugombea urais Jumapili iliyopita nchini Senegal zimekwishakuhesabiwa, matokeo yanaonesha dhahiri uwezekano wa kuwepo Duru ya pili ya Uchaguzi huo baada ya mshindi wa moja kwa moja kushindwa kupatikana hadi hivi sasa. Matokeo hayo yanaonesha rais wa aliyepo madarakani Bw.Abdoulaye Wade akiongoza kwa asilimia 32.17 huku mpinzani wake wa karibu na waziri mkuu wa zamani wa nchi hiyo Bw.Macky Sall akimfuatia kwa kura 25.24, ilhali mshindi akihitajika kuwa na asilimia 50 au zaidi ya kura zote.


Rais Wade ambaye alijitapa kuibuka mshindi siku ya jumapili alipomaliza kupiga kura, amekiri kuwa mambo ni magumu na kusema yote yanawezekana ya pengine yeye kushinda moja kwa moja  au kuingia duru ya Pili na mpinzani wake mkuu Bw. Sall, Huku msemaji wake hapo jana  akikiri  kuwa kweli hali ipo wazi kuwa uchaguzi huo utaingia duru ya pili. Matokeo toka wilaya 282 kati ya jumla ya wilaya 551 yamekwishahesabiwa na yanaendelea kutangazwa katika vyombo mbali mbali vya habari nchini humo huku tume ya taifa ya uchaguzi nchini humo ikisubiri kuyatangaza rasmi siku ya Ijumaa hii.

Ikiwa uchaguzi huo utaingia duru ya pili hiyo itakuwa ni habari mbaya kwa Rais Wade ambaye sasa atakwenda kupambana na wapinzani waliounganisha nguvu zao kumuunga mkono mpinzani mwenzao Bw. Sall.
 Senegal ambayo inaaminiwa kuwa nimoja ya nchi zenye demokrasia barani Afrika imeingia dosari hivi karibuni baada ya rais wa nchi hiyo aliyepo madarakani Bw.Abdoulaye Wade kung'ang'ania kugombea katika awamu ya tatu baada ya kumaliza vipindi vyake viwili vya uongozina kusababisha  vurugu pamoja na maandamano yaliyoshuhudia matumizi ya nguvu kutoka kwa vikosi vya Usalama hali inayolaaniwa na Wanaharakati na Wapinzani nchini humo.
Hata hivyo ucrudiaji wa uchaguzi huo ni suala la kusubiri kwani kwa sasa lolote laweza kutokea na pengine mshindi wa moja kwa moja akapatikana.














MAANDAMANO YATISHIA UCHAGUZI SENEGAL

VIONGOZI WA DUNIA WAKUTANA LONDON KUJADILI HALI YA SOMALIA.


LONDON, UINGEREZA.
Viongozi mbalimbali duniani wanakutana leo hii Mjini London Uingereza kujadili hatima ya Somalia. Viongozi hao wanakutana na viongozi wa serikali ya Somalia kutafuta namna ya kuunganisha nguvu dhidi ya Uharamia, Umasikini uliokidhiri, njaa na Vita ya wenyewe kwa wenyewe nchini Somalia.
Takribani nchi 40 zimetuma wawakilishi katika mkutano huo huku Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bi.Hillary Clinton na Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon wakiwa miongoni mwa wahudhuriaji.Wahudhuriaji wengine ni Umoja wa Ulaya, Umoja wa Afrika, na Umoja wa Nchi za Kiarabu.

Hata hivyo kikundi cha waasi wa Al-Shabab kinachopigana kuipinga Serikali ya Somalia hakijawakilishwa katika Mkutano huo, huku kiongozi wake kamanda Abu Abudurehman akionya kuwa ikiwa matokeo ya mkutano huo yatakuwa ni uingiliaji wa mambo ya Somalia basi utapelekea hali mbaya zaidi nchini humo.
Uingereza ambayo ndiyo nchi mwenyeji na muandaaji wa mkutano huo imesema lengo la mkutano huo ni kukutanisha, na kuunganisha nguvu za pamoja za kimataifa juu ya Somalia.
Mkutano wa aina hii uliwahi kufanyika miaka 20 iliyopita na kupelekea kuongezeka kwa misaada ya kimataifa nchini Somalia ingawa haujafanikiwa kuleta mabadiliko makubwa mpaka sasa.
Somalia imekuwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa miaka mingi tangu kuangushwa kwa Utawala wa kiditekta wa Bw.Siad Barre mwaka 1991, ambapo kwa mujibu wa Shirika la msalaba mwekundu zaidi ya watu Milioni Moja wameuawa kutokana na vita hiyo.
Kwa sasa Nchi hiyo ina serikali dhaifu chini ya Rais Sheikh Sharif Sheik Ahmed ambayo inadhibiti baadhi ya maeneo tu ya nchi hiyo huku ikikabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa kundi la Al-shabab.
Lengo kuu la mkuatano huo litakuwa ni Usalama, njaa, lakini kitu muhimu ni nini kitafuata baada ya mkutano huo ikizingatiwa kuwa serikali iliyopo madarakani ilishamaliza muda wake tangu mwezi Agosti mwaka jana.Pengine wasomalia wasubiri nini kitaamuliwa kwani labda wakati huu kunaweza kuwa na matumaini na hali ikawa tofauti na yale yaliyojiri baada ya lundo la mikutano iliyokwishafanyika juu ya Somalia.


WAANGALIZI WA UMOJA WA MATAIFA WAONDOKA IRAN


VIENNA/TEHRAN |
Waangalizi wa umoja wa mataifa waameondoka leo nchini Iran baada ya kukataliwa na Iran kukagua maeneo muhimu ya siri yanayohisiwa kutengeneza silaha za Nyuklia hali ambayo inaweza kuongeza mvutano kati yake na mataifa ya Magharibi.
Marekani imeishutumu Iran na kusema kwa mara nyingine tena nchi hiyo imeka
taa kutimiza wajibu wake wa kimataifa katika mpango wake huo wa nyuklia.


Iran kwa upande wake kupitia kwa kiongozi mkuu wa kidini Bw.Ayatollah Ali Khamenei Imesema sera za iran kuhusu mpango wake wa nyuklia hazitabadilika licha ya mkandamizo kutoka kwa nchi za magharibi zinazoutuhumu mpango huo kama wa kutengeneza silaha
za maangamizi, "Kwa msaada wa Mungu na bila kujali propaganda, mpango wa nyuklia wa iran utaendelea kwa uimara na Umakini" alisema kiongozi huyo akiongeza kuwa vikwanzo na mauaji hayatazaa matunda katika kuukwamisha mpango huo.


Timu ya wataalamu kutoka Vienna ya kuchunguza Nguvu za atomiki IAEA ilikuwa nchini Iran ikitegemea kukagua sehemu ya Parchin ambapo ndipo kunaaminika kuwepo kwa vifaa vya majaribio ya milipuko lakini IAEA imesema Iran imewazuia kufika sehemu hiyo.
Kukataliwa huko timu hiyo kunaweza kuongeza msuguano zaidi na hati hati ya kuvunjika kwa kwa mapatano ya mradi huo wa nyuklia kati ya Iran na mataifa sita yakiwemo Marekani,China, Uingereza, Urusi,Ufaransa na Ujerumani.