Tuesday, March 05, 2013

UCHAGUZI KENYA-POLISI AMPIGA RISASI MSIMAMIZI WA KITUO CHA KURA

Murang'a-KENYA,
 Katika hali isiyo ya kawaida polisi mmoja amemuua msimamizi wa kituo cha kupigia kura Bw.Waithanje Mwaniki katika jimbo la Kangema walipokuwa njiani wakirudi kutoka katika kituo cha kupigia kura na masanduku ya kura. 

Taarifa ya awali iliyotolewa na Mkuu wa wilaya hiyo imesema polisi huyo alikuwa ndani ya gari na marehemu akiwa amekaa kiti cha nyuma ya Marehemu na alimpiga risasi hiyo kwa bahati mbaya.

Polisi huyo amekamatwa na uchunguzi ukiendelea ambapo utata zaidi umeligubika tukio hilo kutokana na msimamizi msaidizi wa kituo hicho kupotea baada ya tukio hilo na haifahamiki yupo wapi mpaka sasa<t>

UCHAGUZI KENYA-MATOKEO YAENDELEA KUTOLEWA-KENYATTA BADO KINARA.

Baada ya siku kashikashi ya uchaguzi na kupiga kura  nchini Kenya, Matokeo ya uchaguzi huo yameazwa kutangazwa toka hapo jana. 

Matokeo hayo mpaka sasa yanaonesha Uhuru Kenyatta anaongoza kwa asilimia hamsini na tano(55%) huku mpinzani wake Raila Odinga akiwa na asilimia arobaini na moja(41%) , Musalia Mudavadi wa Peace Coalition asilimia 3 na vyama vingine vikipata asilimia 1 na vingine chini ya asilimia 1.

Wananchi wa Kenya Wakifuatilia matokeo hayo katika Televisheni.






       Ufuatao ni Muhtasari wa matokeo hayo:
  • Uhuru Kenyatta (Jubilee Alliance): 55%
  • Raila Odinga (Coalition for Reform and Democracy): 41%
  • Musalia Mudavadi (Peace coalition): 3%
  • Asilimia 37% ya vituo vya kupigia kura vimeshatoa matokeo.