NEW YORK-MAREKANI
Mwanaume mmoja aliyetambulika kwa jina la Terence Tyler, (23) amewapiga na kuwaua wafanyakazi wanzake kwa risasi na kujiua mwenyewe katika duka la New Jersey wanapofanya kazi leo hii mjini nje kidogo ya Jiji la New York huko Marekani.Waliouawa wametambuliwa kuwa ni binti wa miaka 18, Cristina LoBrutto na kijana Bryan Breen mwenye umri wa miaka 24.
Wafanyakazi wenzake walifunga milango wakati akirudi ingawa alifanikiwa kuwapiga risasi kupitia dirishani.
Tukio hilo ambalo limetokea kabla ya kufunguliwa duka hilo, limekuwa ni mwendelezo wa matukio ya upiganaji risasi nchini humo baada ya lile lililotokea katika jumba la makumbusho la Sikh temple ambapo watu 6 waliuawa pamoja na lile lililotokea katika filamu ya Batman ambapo watu 12 waliuawa hali inayoongeza shinikizo juu ya sheria za uuzaji wa silaha nchini Marekani.
No comments:
Post a Comment