dekdee
Saturday, February 28, 2015
Thursday, February 12, 2015
KUMBE HII NDIYO SABABU YA MSANII LADY JAYDEE KUTOFANYA COLABO NA WASANII WA KIKE
Posted by
Chiefwire
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiQOItywmuly4RcaByYVRoIICgwnnfkFJg5GFwUN8cna4QkOze5Ios54USuGyTwetLLW6qR7gMhGed8kLjNzhXfjdUYZmh7v-50_Z8tObR1EGcECZNNS_uED8hB0Rexo-tkb0iNrhBZIcMY/s1600/karibuni.jpg)
Lady Jaydee ametoa nafasi kwa mashabiki na followers wake wa Instagram kumuuliza maswali na kuahidi kuyajibu. Miongoni mwa maswali mengi aliyoulizwa ni pamaoja na kwanini hafanyi collabo na wasanii wa kike, na kuhusu Ugomvi / Tofauti na watu (wasanii) /Radio na mpango wa kupatana nao.
“Duuuh maswali yako mengi sana karibia 300 Ila ki ukweli yote yanafanana So, what i will do I will pick top 10 ya maswali yaliojirudia, halafu nitalijibu moja baada ya jingine. Watu wooote nikiwakusanya, maswali yenu hayazidi 10, Leo mtaelewa kwanini sijibu comments. Sababu nikifanya hivyo itabidi niache kazi zote, Kaeni tayari kwa majibu, moja baada ya jingine” aliandika Jaydee kabla hajaanza kuyajibu.
Haya ni baadhi ya maswali na majibu.
Swali: Kwanini sifanyi collabo na wasanii wa kike?
Jibu :
“Nimewahi kufanya na wasanii mbali mbali wa kike ila sijui kwanini hamjaziskia.
1.Mwasiti amewahi kunishirikiisha
2. Nimewahi kumuandikia na kushiriki kuimba kwenye wimbo wa movements za Albino na Kaysha
3. Nimewahi kumwandikia na kushiriki kuimba nae Nakaaya Sumari
4. Nimewahi kumwandikia wimbo Patricia Hillary
5. Nimewahi kumshirikisha RAY C kwenye wimbo wangu toka Album ya Machozi unaitwa, Nimekubali na wapo wasichana mbali mbali waliopita Machozi Band na kujifunza kuimba leo mnawafahamu.
Kumbukeni tu kuwa kutoka kwa mtu itategemea na nyimbo zake kuwa promoted redioni na mimi sio mwenye hizo redio.
Msaada pekee ni kushiriki kila ntakapotakiwa kufanya hivyo”
Swali: Ugomvi / Tofauti na watu Artists /Radio Na mpango wa kupatana nao
JIBU :
“Nitapatana na mtu atakae kubali kuwa alikosa, km naamini yeye ndio alinikosea itabidi aniombe msamaha. Kama mimi ndio nilikosa nitaomba pia msamaha,Otherwise hakuna miujiza.Siwezi kumuomba mtu msamaha endapo naamini kabisa sijakosa .
Niliowahi kuwakosea nilishawaomba msamaha wooote.Hakuna binadamu asie kosea Ila siwezi ku surrender kiuongo au kwa uoga wa maisha.
Naamini hata nikiuza nyanya bado wapo watu wanaohitaji nyanya, na watanunua. Je! Hili jibu limejitosheleza?.Naamini hata nyinyi mmewahi kutofautiana na watu wenu wa karibu.
Kukubali kosa ndio mpango”
Swali: Siasa
Mchango katika jamii
JIBU:
“Sio mpenzi na sitegemei kujihusisha na siasa, wala chama chochote. Kila binadamu ana mchango katika jamii kwa njia moja au nyingine, Direct au indirect.
Ukitambua moja lolote nililowahi kulifanya likakupa furaha ndio mchango wangu, samahani kwa yaliokuudhi.
Swali la 4 mpk la 10 ntamalizia kesho, yasipoisha hata kesho kutwa.Najua kuna maswali mazito mnayosubiria majibu, yale ya kidaku zaidi. …Na mimi kwa kuwarusha roho nayaweka mwiiiishooo.Yatajibiwa tu, msitie shaka. …”
Friday, February 06, 2015
Vanessa Mdee na Barnaba wamekutana tena, hizi ni picha za utengenezaji wa video yao mpya.
Posted by
Unknown
Vanessa Mdee na Barnaba Elias Feb 6, waliingia location kumalizia utengenezaji wa video mpya ya single yao iitwayo Siri, video hiyo imeongozwa na Hanscana kwenye kijiji cha Makumbusho Dar es Salaam.
Hizi ni baadhi ya picha ambazo nimekuchukulia baada ya kushuhudia utengenezaji wa video hiyo mpya, zicheki hapa zote mtu wangu.
Picha,Jibu la Kim Kardashian kuhusu watu anaotaka kupiga nao SELFIE, utashangaa.
Posted by
Unknown
Wednesday, February 04, 2015
Tuesday, February 03, 2015
Huyu amewekewa mikono ya mtu mwingine!
Posted by
Chiefwire
Madaktari katika Chuo cha Tiba cha Amrita, Kochi huko India wamefanikiwa kufanya upasuaji wa aina yake wa kupandikiza mikono mipya kwa binadamu aliyekatika viungo hivyo.
Upandikizaji huo uliofanyika Januari 12 na 13, ulifanikiwa kwa mara ya kwanza, baada mwanamume mwenye umri wa miaka 30, aliyekatika mikono katika ajali ya treni kuwekewa mingine ambayo ilichukuliwa kutoka kwa kijana wa miaka 24 aliyefariki katika ajali ya gari.
Mkuu wa kitengo cha upasuaji katika chuo hicho, Prof. Subramania Iyer alisema: “Siku 14 baada ya upasuaji, mikono ilikubaliwa na mwili na ikaanza kujongea, yaani aliyepandikizwa aliweza kuisogeza huku na kule. Mgonjwa alitolewa chumba cha wagonjwa mahututi na huduma nyingine za kumchunguza ziliendelea.”
Daktari katika Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Hospitali ya Muhimbili (Moi), Prof. John Kahamba aliliambia Gazeti la MWANANCHI kuwa hiyo si mara ya kwanza kwa upandikizaji wa mikono kufanyika duniani kwani ina tofauti kubwa na upandikizaji wa figo au ini.
Profesa Kahamba alisema upasuaji huo unafanyika kwa kuhakiki mambo mbalimbali ikiwamo uwiano wa kundi la damu, uhai wa seli na misuli na mishipa midogo ya fahamu.
Profesa Kahamba alisema kama upandikizaji wa figo unavyofanyika, kadhalika upandikizaji wa mikono unahitaji umakini wa muda.
Anasema iwapo utachelewa kuunganisha mikono baada ya kuitoa, seli zake zinaweza kufa na kushindwa kufanya kazi zitakapopandikizwa kwenye mwili.
Friday, January 30, 2015
Polisi wamkatama Wema Sepetu
Posted by
Chiefwire
Tukio hilo lilitokea Jumanne iliyopita, nyumbani kwa mwigizaji huyo, Kijitonyama jijini Dar kulikokuwa na bethidei ya rafiki yake aliyejulikana kwa jina moja la Neema.
Awali, mapaparazi wa GPL walipokea simu ya mmoja wa majirani wa Wema ambaye alidai mwigizaji huyo amekuwa na tabia ya kufanya sherehe kwake na kufungulia muziki mkubwa ambao unasababisha kero.
“Kwa kweli ni kero, kila mara amekuwa na tabia ya kupiga muziki mkubwa katika sherehe zake ambazo hazina kichwa wala miguu. Kama jana (usiku wa Jumatatu) muziki ulifunguliwa kuanzia saa mbili usiku mpaka asubuhi na majirani walimfuata Wema mara kadhaa kumtaka apunguze sauti lakini aliwajibu vibaya.
“Njooni mshuhudie wenyewe, tumeita polisi wamkamate,” alisema jirani mmoja.
Mapaparazi wetu walichukua usafiri wa pikipiki na kuwahi fasta na kukuta polisi wakihangaika kwa muda mrefu kumkamata mrembo huyo lakini ikashindikana kwa kuwa alikuwa amelewa na kukimbia hovyo huku akiwa nusu utupu.
“Kwa sababu hiyo walimkamata mmiliki wa muziki ambaye jina lake halikupatikana mara moja na mwenye sherehe (Neema) kisha kwenda nao katika ofisi za mtendaji, Kijitonyama kwa ajili ya hatua za kisheria,” alisema.
Akizungumza na GPL, mwenyekiti wa mtaa huo, Mzee Haogwa, alithibitisha kuletewa malalamiko ya Wema na kufika nyumbani hapo ambapo pia alidai alishangazwa na kitendo cha kuwakuta wanaume tata kwenye sherehe hiyo.
Picha: Timu iliyofika nyumbani kwa Wema Sepetu kumkamta kwa usumbufu aliosababisha kwa majirani.Wakachikua spika na kumbeba mwenye sherehe, Neema( rafiki wa Wema Sepetu) kwenye bajaji.GPL
Monday, January 26, 2015
MKE WA WAZIRI MKUU MAMA TUNU PINDA ATUNIKIWA SHAHADA YA UZAMILI YA USIMAMIZI WA MIRADI.
Posted by
Chiefwire
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Asha-Rose Migiro akimtunuku shahada ya uzamili ya usimamizi wa miradi mke wa Waziri Mkuu mama Tunu Pinda katika mahafali ya 27 ya chuo hicho yaliyofanyika mjini DODOMA. Kushoto anayeshuhudia ni Makamu mkuu wa chuo hicho
Profesa Tolly Mbwete.
Mke wa Waziri Mkuu mama Tunu Pinda akitoka kupokea shahada ya uzamili ya usimamizi wa miradi. Akiongea baada ya hapo Mama Pinda ametoa wito kwa kinamama wa Tanzania na Afrika kwa jumla kujiendeleza kielimu ili kukomboa mataifa yako kutoka katika dimbwi la umaskini
Kikundi cha wake wa viongozi kutoka Dar es salaam kikimpongeza mlezi wao Mama Tunu Pinda kwa kutunukiwa shahada ya uzamili ya usamamizi miradi ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania katika mahafali ya 27 iliyofanyika Mjini Dodoma. Toka kushoto ni Mama Mashiba, Mama Lukuvi na Mama Malima .
Subscribe to:
Posts (Atom)